Taarifa ya shughuli za Mkutano wa 9 wa Baraza la Kumi la Wawakilishi

Posted on: 21.11.2022
Mkutano wa Nane wa Baraza la Kumi la Wawakilishi Zanzibar unatarajiwa kuanza siku
ya Jumatano tarehe 23 November, 2022, saa 3:00 asubuhi.
A: SHUGHULI ZA BARAZA:
Shughuli za Mkutano huo zitakuwa kama ifuatavyo:-
- Maswali na Majibu.
Afisi ya Baraza la Wawakilishi imepokea na kuratibu maswali 138 kwa ajili ya Mkutano huu. - Miswada ya Sheria.
Miswada ya Sheria iliowasilishwa na kusomwa mara ya kwanza katika Mkutano wa September 2022, itasomwa kwa mara ya pili na kujadiliwa katika Mkutano huu wa Tisa , Miswada yenyewe ni:-
i. Mswada wa Sheria ya kufuta Sheria ya Watu wenye ulemavu (Haki na
Fursa), Nam. 9 ya 2006 na kuweka masharti yanayohusiana na watu wenye ulemavu na mambo mengine
yanayohusiana na hayo.
ii. Mswada wa Sheria ya kurekebisha Sheria ya Chuo cha Utawala wa Umma Nam 1 2007 na mambo mengine yanayohusiana na
hayo. - Miswada kwa hati ya Dharura.
- i. Mswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbali mbali
- ii. Mswada wa Sheria ya kufuta Sheria ya Bodi ya Mapato na Kutunga Sheria mpya ya Bodi ya Mapato Zanzibar.
- Taarifa ya Serikali Taarifa hii itahusu uwasilishwaji wa Ripoti ya Sita ya Utekelezaji wa kazi za Tume ya Maadili kwa mwaka 2021/2022