Taarifa ya shughuli za Mkutano wa 14 wa Baraza la Kumi la Wawakilishi

Posted on: 12.02.2024

Mkutano wa Kumi na Nne wa Baraza la Kumi la Wawakilishi Zanzibar unatarajiwa kuanza siku ya Jumatano ya tarehe 14 Februari, 2024, saa 3:00 asubuhi.

A: SHUGHULI ZA BARAZA

Shughuli za Mkutano huo zitakuwa kama ifuatavyo:


1. Maswali.

Afisi ya Baraza la Wawakilishi imepokea na kuratibu maswali 181 kwa ajili ya Mkutano huu.


2. Uwasilishwaji wa Ripoti za Kamati za Kudumu za Baraza la Wawakilishi kwa Mwaka 2023/2024.

 

3. Miswada ya Sheria.

 

Miswada miwili ambayo ilisomwa kwa mara ya kwanza katika Mkutano kilichopita, itasomwa kwa mara ya pili na kujadiliwa katika kikao hiki; miswada hiyo ni:-

 

i)             Mswada wa Sheria ya Kufuta Sheria ya Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar, Nam. 12 ya 2019 na Kutunga Sheria ya Mamlaka ya Serikali Mtandao Zanzibar Kusimamia Huduma za Serikali Mtandao Zanzibar na Mambo Mengine yanayohusiana na hayo.

 

ii)            Mswada wa Sheria ya Kufuta Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar. Nam. 3 ya 2011 na Kutunga Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Zanzibar kwa ajili ya Kutoa Msaada wa Kifedha wa Wanafunzi na Mambo Mengine yanayohusiana na hayo.


4. Taarifa ya Wabunge watano (5) wanaoliwakilisha Baraza katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.

5. Ripoti ya Mapendekezo ya Muelekeo wa Mpango wa Taifa.


       6. Ripoti ya Utekelezaji wa Maoni, Ushauri na Mapendekezo ya Kamati ya Kuchunguza na Kudhibiti Hesabu za Serikali (PAC) kwa mwaka 2020/2021.


        7. Ripoti ya Mwaka ya Mamlaka ya Dawa za Kulevya, Zanzibar 2022/2023.

//