Taarifa ya shughuli za Mkutano wa 13 wa Baraza la Kumi la Wawakilishi

Posted on: 27.11.2023

Mkutano wa Kumi na Tatu wa Baraza la Kumi la Wawakilishi Zanzibar unatarajiwa kuanza siku ya Jumatano tarehe 29 Novemba, 2023, saa 3:00 asubuhi.

 

SHUGHULI ZA BARAZA

Shughuli za Mkutano huo zitakuwa kama ifuatavyo:-


1.   Kiapo cha Uaminifu cha Mjumbe.

Mwakilishi Mteule wa Jimbo la Mtambwe Mhe. Mohamed Ali Suleiman ataapishwa kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi.

 


2.   Maswali na Majibu.

Afisi ya Baraza la Wawakilishi imepokea na kuratibu maswali 88 kwa ajili ya Mkutano huu.

 


3.   Miswada ya Sheria.

Miswada ya Sheria iliyowasilishwa na kusomwa kwa mara ya Kwanza katika Mkutano wa mwezi Septemba, 2023 itasomwa kwa mara ya pili na kujadiliwa katika Mkutano huu wa Kumi na Tatu. 

 

Miswada yenyewe ni:-

 

1.    Mswada wa Sheria ya Kufuta Sheria ya Kuanzisha Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Nam. 11 ya 2003 ya Kutunga Sheria ya Ukaguzi wa Umma na Kuweka Mambo Mengine Yanayohusiana na Hayo.


2.    Mswada wa Sheria ya Kufuta Sheria ya Mahakama ya Kadhi Nam. 9 ya 2017 na Kutunga Sheria ya Mahakama za Kadhi na Kuweka Mambo Mengine Yanayohusiana na Hayo.


3.    Mswada wa Sheria ya Kuweka Masharti ya Utoaji Leseni, Kudhibiti na Kusimamia Biashara ya Huduma Ndogo Ndogo za Fedha Kwa Ajili ya Kudumisha Utulivu, Usalama na Ubora wa Huduma Ndogo Ndogo za Fedha na Mambo Mengine Yanayohusiana na Hayo.

 

 

4.    Mswada wa Sheria ya Kufuta Sheria ya Mamlaka ya Kukuza na Kulinda Uwekezaji Zanzibar, Nam. 14 ya 2018 na Kutunga Sheria ya Uwekezaji Zanzibar na Kuweka Masharti Mengine Yanayohusiana na Hayo.

 

5.    Mswada wa Sheria ya Kuanzisha Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini Zanzibar na Kuweka Mambo Mengine Yanayohusiana na Hayo.

 

6.    Mswada wa Sheria ya Kuanzisha Wakala wa Bohari Kuu ya Dawa Zanzibar kwa ajili ya Ununuzi, Utengenezaji, Uhifadhi na Usambazaji wa Dawa na Mambo Mengine Yanayohusiana na Hayo.



4.   Taarifa ya Serikali kuhusu Ripoti ya Saba ya Utekelezaji wa kazi za Tume ya Maadili kwa mwaka 2022/2023

//