Taarifa ya shughuli za Mkutano wa 19 wa Baraza la Kumi la Wawakilishi

Posted on: 05.05.2025
Mkutano
wa Kumi na Tisa wa Baraza la Kumi la Wawakilishi Zanzibar unatarajiwa kuanza
siku ya Jumatano tarehe 07 Mei, 2025, saa 3:00 asubuhi.
A: SHUGHULI ZA BARAZA:
Shughuli
za Mkutano huo zitakuwa kama ifuatavyo:-
1.
Maswali na Majibu.
Afisi
ya Baraza la Wawakilishi imepokea na kuratibu maswali 311 kwa ajili ya
Mkutano huu.
2.
Majadiliano ya Bajeti ya Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
3.
Miswada ya Sheria.
Miswada
miwili ya Sheria itawasilishwa na kujadiliwa, Miswada yenyewe ni:-
i.
Mswada
wa Sheria ya Fedha (Finance Bill)
ii.
Mswada
wa Sheria ya Kuidhinisha Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2025/2026.
4. Kuvunjwa kwa
Baraza la Kumi la Wawakilishi, Zanzibar.